Mabingwa Watetezi wa Afcon Algeria jana walianza kutetea ubingwa wa michuano hiyo kwa suluhu dhidi ya Sierra Leone mchezo wa kundi E.



Tofauti na matarajio ya wengi Algeria imeshindwa na kuondoka na alama tatu baada ya Sierra Leone kuonyesha moyo wa kujituma na kuizua safu ya Ushambuliaji ikiongozwa na Riyad Mahrez anayechezea Manchester City ya England na Yacine Brahimi.

 

Shujaa wa mchezo huo alikuwa mlinda mlango wa Sierra Leone Mohamed Kamara ambaye aikuwa mchezji bora wa mechi hiyo akizuia michomo mingi na kuiweka timu yake salama.

Mohammed  Kamara wa Sierra Leone alifanya aliokoa michomo  saba katika mechi dhidi ya Algeria, na kuweka rekodi ya  golikipa aliyefanya saves nyingi zaidi katika AFCON bila ya kuruhusu goli tangu Ovono wa Equatorial Guinea afanye hivyo katika mechi dhidi ya DR Congo mwaka 2015.

 

Suluhu hiyo inaifanya Algeria kufikisha mechi 35 bila kufungwa wakiifukuzi rekodi ya mabingwa wa ulaya Italia ya michezo 37 bila kufungwa.