Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa na  klabu ya RB Leipzig Christopher Nkunku atakosa fainali za kombe la dunia nchini Qatar baada ya kuumia mazoezini akiwa na timu ya taifa.


 

Nkunku amepata majeraha amepata majeraha ya Mguu kufuatia kuchezewa Tackling mbaya na kiungo wa Real Madrid Camavinga ameumia siku nne kabla ya kuanza rasmi kwa fainali hizo Jumapili  Novemba 20, 2022.

Kikosi cha Kocha Didier Deschamps tayari kinamajeruhi  kadhaa ambao watazikosa fainali hizo akiwemo Kiungo wa Chelsea N'Golo Kante  na kiungo wa Juventus Paul Pogba.

Mabingwa watetezi Ufaransa itafungua dimba dhidi ya  Austaralia Jumanne Novemba 22.