Klabu ya Arsenal inajiandaa kumpa mkataba mpya wa miaka miwili meneja wa timu hiyo Mikael Arteta ili kuendelea kuinoa timu hiyo baada ya bodi ya the gunners kuridhika na uwezo alionyesha tangu achukue mikoba ya Unai Emery miaka miwili iliyopita.
Mabosi wa Arsenal wamefurahia
mpango wa Arteta kuwatumia vijana zaidi
kwenye kikosi hicho pamoja usimamizi mzuri wa nidhamu kwa wachezaji wenye
majina makubwa.
Mkataba wa sasa wa Arteta
unaisha mwakani 2023, na kumekuwa na tetesi kuwa Manchester City wanamuona kama
mtu sahihi wa kumridhi Pep Guardiola ambaye huenda akaondoka City baada ya
mkataba wake kuisha mwakani.
0 Maoni