Leo usiku saa 2:15 itapigwa fainali ya kombe la Mapinduzi 2022 kati ya Azam Fc dhidi ya Mnyama Simba kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar.



 

 

Azam wamingia fainali baada ya kuwatoa mabingwa watetezi Yanga kwa mikwaju ya penati 9-8 baada ya dakika 90 kumalizika kwa suluhu, huku Simba ikiitungua Namungo Fc kwa magoli 2-0.

 

Historia inaonyesha hii itakuwa fainali ya Nne, tatu zilizopita wana lamba lamba Azam fc wameibuka washindi na kuondoka na kombe.

 

Je leo Azam ataendeleza ubabe mbele ya Simba? Au Mnyama atafuta uteja na kuibuka na ushindi tusuburi dakika 90 zitaamua.