Huenda huu ukawa msimu mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa kwa Barcelona baada ya jana Januari 20, kutolewa kwenye hatua ya 16 bora ya Copa de Rey dhidi ya Athletic Club baada ya kuchezea kichapo cha mabao 3-2.

 


Iker Muniain  alikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za Barcelona mapema tu dakika ya 2’ Barca wakasawazisha kupitia kijana waliyemsajili kutoka Manchester City,  Ferran Torres dakika ya 20.

 

Inigo Martnize akaipa uongozi Athleti Club dakika ya 86, vijana wa Xavi Hernandez wakarudi mchezonu baada ya Pedri kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 2-2 dakika 90+3, Muniain kwa mara nyingine akaipa ushindi Athletic kwa bao la Mkwaju wa Penati kwenye dakika 30 za nyongeza (Etra Time)

 

Msimu huu Barcelona  wameondolewa kwenye Copa del Rey raundi  16 kwa kufungwa 3-2 na Athletic Bilbao,  Wametolewa hatua ya makundi Uefa Champions League na sasa wanashiriki Ueropa League, wameondolewa kwenye nusu fainal ya Super Cup na mahasimu wao wakubwa Real Madrid na sasa wapo nafasi ya 6 kwenye msimamo wa La Liga.