Klabu ya Barcelona inawinda Saini ya kiungo mshambuliaji wa Manchester United Bruno Fernandes iwapo watashindwa kumpata kinda wa Erling Haaland.

 


Tangu alivyofunga hat-trick dhidi ya Wolves mwanzoni mwa msimu huu  kiwango Fernandes kimekuwa cha kushuka nakupanda akifunga magoli mawili tu kwenye michezo 16.

 

Mapema wiki hii Rais wa Barca   Joan Laporta alikaririwa akisema wanajuandaa kuishangaza dunia kwani wanataka kushusha wachezaji wakubwa kwenye dirisha la usajili.

 

Staa huyo wa Ureno amekuwa mchezaji muhimu kwa United kwa misimu miwili amefunga magoli 45 asisti 34 kwenye michezo 105

 

Tangu kuwasili kwa Cristiano Ronaldo Bruno ameshuka kiwango akifunga magoli 5 kwenye michezo 18 ya Epl.