Staa Zambia wa
Klabu ya Simba, Clatous Chota Chama, amewasili nchini jioni na hii ya leo
Januari 14, 2022 na kutambulishwa rasmi kujiunga
tena na mabingwa hao wapya wa Mapinduzi Cup na Mabingwa watetezi wa Kombe la
Ligi Kuu ya Nbc.
Triple C amejiunga na Simba akitokea Rs
Berkane ya Morocco kwa mkataba wa miaka miwili na amewakili katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akitokea kwao Zambia.
Chama aliondoka
Simba Augusti 13, 2021 na kujiunga na RS Berkane ya Morocco na sasa
anarejea baada ya kudaiwa kushindwa kuzoea mazingira nchini Morocco.
Berkane imesema sababu kubwa ya Chama kuondoka Morocco ni
kushindwa kuzoea mazingira ya nchi hiyo kwa haraka pamoja na masuala ya
kifamilia.
0 Maoni