Mabingwa wa Ulaya Chelsea, jana usiku Januari 18, wameshindwa kufurukuta mbela ya Brighton & Hove Albion baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 katika mchezo wa ligi kuu England uliochezwa katika dimba la Amex, England.

 


Vijana wa Thomas Tuchel walikuwa wa kwanza kutikisa nyavu kupitia Hakim Ziyech kipindi cha kwanza dakika ya 28' kabla ya Adam Webster's kuzawazisha kwa kichwa dakika ya 60 kipindi cha pili

 

Sare  hiyo imeifanya The Blues  kufikisha alama 44 na hivyo kuachwa alama 12 na vinara wa ligi Manchester City wenye pointi 56.


 Katika mechi nne za mwisho Chelsea imeshindwa kupata ushindi ikitoa sare tatu na kipigo kimoja kutoka kwa Manchester City.