Chelsea imetinga hatua ya fainali ya kombe la Carbao Cup baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspur mchezo wa nusu fainali ya pili  na kufanya matokeo ya jumla kuwa 3-0 mchezo uliopigwa usiku wa kuamkia Januari 13.

 


Goli pekee la The Blues limefungwa na mlinzi Antonio Rudiger dakika ya 18 ya mchezo  kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona na kuipa uhakika Chelsea kucheza fainali katika uwanja wa Wembely.

 

Chelsea inasubiri mshindi kati ya Liverpool na Arsenal ambao wanashuka dimbani leo Januari 13.