Novak Djokovic  atatetea  michuano ya wazi ya Australia *Austaralia Open) 2022  licha ya kuwa hajapata chanjo ya UVIKO-19 baada ya Mahakama ya Australia kuwa mchezaji namba moja kwa ubora Duniani kwenye Tenisi, kuachiliwa huru na kwenda kushiriki michuano hiyo.



 

Hakimu wa kesi hiyo amesema kuwa ameona kuwa hakuna madai yoyote ya msingi kufuatia kuzuiliwa kwa hati ya kusafiria ya Djovo na Ofisa wa mpakani katika uwanja wa ndege wa Melbourne.

Jaji Antony Kelly ameamua hati ya kusafiria aliyokuwa anatumia Djokovic ni halali na anaruhusiwa kuingia nchini Australia ilikuweza kuweza kushiriki mashindano ya wazi ya Australia.

Mashindano ya Australia Open yanatarajia kuanza Januari 17, ambapo Djokovic anaingia kwenye michuano hiyo kama bingwa mtetezi akiwa ameshinda taji la Grand Slam  mara tisa.