Klabu ya Everton ya England imemtimua kazi kocha wake Rafael Benitez baada ya mfululizo wa matokeo yasioridhirisha kwenye mechi za ligi kuu ya Epl.

 


Benitez anaingia kwenye historia ya klabu hiyo kwa kuwa kocha aliyefundisha muda mchache akichukua timu hiyo mwezi Juni 2021 akidumu kwa miezi mitano tu, Rafa alichukua nafasi hiyo ambayo iliachwa wazi na Carlo Anchelotti aliyetimkia Real Madrid.

 

Mchezaji wa zamani wa timu hiyo aliyewika na Manchester United, Wayne Rooney anapewa nafasi ya kuchukua mikoba ya Benitez.