Kufuatia  matokeo mabaya ya timu ya Taifa  Ghana katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika inayoendelea, Wizara ya michezo ya nchi hiyo katika mkutano wa dharura siku ya Ijumaa iliagiza Chama cha Soka cha Ghana kumfukuza kazi kocha wake Mserbia, Milovan Rajevac.



 Rajevac  kwa  kipindi chake cha kwanza akiwa na Black Stars aliiongoza Ghana kutinga fainali za AFCON 2010 na Robo fainali ya Kombe la Dunia la 2010.


Alirejea Septemba 2021  katika  awamu yake ya pili hakikwenda kama ilivyotarajiwa kwani Ghana walitoka AFCON 2021 bila kupata  ushindi, na kuandika mpya kwa  Black Stars.