Simba leo Januari 26, imepoteza mechi ya pili msimu huu kwenye ligi ya NBC,  baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar, mchezo uliochezwa uwanja wa Kaitaba Bukoba mkoani, Kagera.

 




Goli la wakata miwa wa Kagera limefungwa na mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Simba Hamis Kiiza  dakika 71 chache baada ya kuingia.

 

Katika mchezo Kiiza alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kuonekana anapoteza muda na awali tayari alikuwa na kadi ya njano.

Licha ya Kocha Pablo kuanza na bila mshambuliaji asilia lakini wachezaji walishindwa kutumia nafasi waliozotengeneza

 

Pengo la pointi limesalia kuwa 10 baina yake na vinara wa ligi watani zao wa jadi Yanga wanaoongoza wakiwa na alama 35 huku Simba akiwa na 25.