Kwa Mujibu wa Daily Mail nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo, atakatwa asilimia 25 ya mshahara wake endapo Manchester United, ikishindwa  kumaliza nafasi ya nne za juu kwenye msimamo wa ligi na hivyo kukosa fursa ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya (Uefa Champions League).

 


Ronaldo amefunga magoli 14 katika mechi 23 tangu arejee United, kwa sasa anapokea mshahara wa paundi laki 385,000 kwa wiki utashuka mpaka paundi laki 288,000

 

United ipo  ya nafasi  saba, pointi mbili nyuma kuifikia West Ham United lakini wapinzani wengine wa Top Four Arsenal na Totenham Hotspur wamecheza mechi pungufu.

Ronaldo alikubali kupunguza mshahara wa paundi 500,000 kwa wiki kutoka Juventus ya Italia lakini bado anabaki kuwa mchezaji anayelipwa mkwanja mrefu akifuatiwa na kipa David de Gea anayelipwa paundi laki 375,000 kwa wiki.