Muda mwingine unaweza kujiuliza kuhusu
mafanikio ya mtu ukadhani labda ni juhudi, kipaji au anachapa kazi sana la
hasha wakati mwingine tunapaswa kungalia kwa jicho la tatu hasa uhusiano wa
huyo mtu na Mungu.
Jumapili ya Januari 16, Mchungaji wa KKKT, Usharika
wa Ubungo Oscar Mlyuka alimwita mbele ya usharika mzima mchezaji wa kimataifa
wa Tanzania Simon Msuva, ambapo amesema
kuwa amezidi kuinuliwa na kuendelea kupata mafanikio kwa sababu hajamuacha
Mungu licha ya umaarufu wake pamoja na mafanikio makubwa aliyokwisha kuyapata.
“Msuva akiwepo nchini hajawahi kukosa kuja
kanisani kwa ibada. Wapendwa washarika na vijana wote kwa ujumla, haijalishi una umaarufu wa kiasi gani
usimwache Mungu, fanya kama Msuva Mungu atazidi kukuinua na kubarika kazi ya
mikono yako” alisema Mch. Mlyuka.
Msuva staa wa timu ya Taifa Stars, anayekipiga
Wydad Casablanca ya Morroco, ameendelea kuipeperusha na kuitangaza vema bendera
ya nchi katika soka kutokana na mafanikio anayoendelea kuyapata huko ughaibuni.
Alianza kuwika na klabu ya Yanga
akafanikiwa kuwa staa mkubwa kwenye kikosi chenye wachezaji nyota kwa wakati
huo kama Donald Ngoma, Obrey Chirwa, Amis Tambwe na Haruna Niyonzima na kufanikiwa kujenga ufalme ndani ya Jangwani.
Kufanya kwake vizuri Yanga kuliwavutia timu
ya Difaa Hassani d'el-Jadida ya Morocco na kumnunua kwa zaidi ya milioni 300
huo ulikuwa mwaka 2017.
Baada ya kuwika sana Jadida, Wydad
wakavutiwa na kiwango cha Msuva na kuamua kuingia benki na kumnunua kwa Tsh.
Bil 1.5 akisaini kandarasi ya miaka minne msimu wa 2020.
Pamoja na juhudi kubwa anazoonyesha kuna
kitu ambacho huenda vijana ambao wanacheza soka na wana ndoto za kufika alipo
Msuva wanapaswa kufahamu.
Vijana mnaomtazama Msuva kama kioo chenu
kuna funzo kubwa hapa, pamoja na juhudi
bidii na kipaji, Tunakumbushwa kumtanguliza Mungu na hata unapopata
cheo, au unapokuwa maarufu usimsahu
Mungu kwani atazidi kuibariki kazi yako.
0 Maoni