Manchester United imeendelea kusususa kwenye ligi kuu ya England baada ya jana usiku kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Aston Villa mchezo uliopigwa katika dimba la Villa Park.

 




Hadi Dakika ya 67 United ilikuwa inaongoza kwa mbao 2-0 magoli yaliofungwa na Mreno Bruno Fernandes dakika ya 6’ na 67’

 

Mabadiliko yaliofanywa na kocha Stven Gerrard ya kumuingiza Phillipe Countinho yalionaekana kuzaa matunda baada ya Jacob Ramsey kupacjhik goli dakika ya 77.

Akicheza mechi yake ya kwanza kwenye uzi wa Villa Countinho, akafunga goli la pili na kuisaidia villa kupata alama  moja muhimu.

Kwa matokeo haya United kwenye msimamo wa Epl  inashika nafasi 7  wakiwa na alama 32, wakati Villa ipo nafasi ya  13 na alama 23.