Manchester United ipo mbioni kuisaka saini Mreno Ruben Neves wa Wolverhampton Wanderers  kwenye dirisha hili dogo ili kuimarisha safu yao ya kiungo.



 

United wapo tayari kutoa Pauni Mil. 35  lakini Wolves wanahitaji kiasi cha pauni 40 ili wamwachie mchezaji huyo.

 

Neves 24, amebakisha mkataba wa miaka miwili ndani Molineux ana ndoto za kucheza michuano ya ligi ya mabingwa ulaya, United wanataka kutumia michuano hiyo ya (uefa) kama chambo kumshawishi kujiunga na Man Utd.