Manchester United  jana usiku Januari 19, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Brentford kwenye mchezo wa ligi kuu ya England uliochezwa jana usiku.

 


Magoli ya United yamefungwa na kinda Antony Elanga dakika ya 55’  ambaye amepachika goli lake la kwanza kwenye Epl, united wakaongeza bao la pili kupitia kwa Mason Greenwood dakika ya  62’ akimalizia pasi safi ya Bruno Fernandes.


Marcus Rashford akitokea benchi aliipa Man United goli la la tatu dakika ya 77’ pasi nyingine ya Fernandes  na kuihakikikishia kuondoka na alama tatu

 

Goli la Brentford limefungwa na Ivany Toney, United bado upo nafasi ya Saba na alama 35