Manchester United imejitoa kwenye kinyang’anyiro cha kumsajili Erling Haaland baada ya nyota kuripotiwa kupendelea kutua Real Madrid.


 


Haaland anavutiwa na Meneja mpya wa Man United Rafl Rangnick lakini matarajio ya klabu hiyo ambayo ipo kwenye kipindi cha mpito pamoja na kuwa hatarini kukosa UEFA msimu ujao kunazima ndoto za kujiunga nayo.


 

Man United inasaka fowadi hatari wa kucheka na nyavu atakayerithi mikoba ya Edson Cavani ambaye huenda akaondoka kwenye timu hiyo majira ya kiangazi.