Wachezaji wa  Yanga  Khalid Aucho, Yanick Bangala, Djuma Shabani na Mukoko Tonombe, watakuwa sehemu ya kikosi cha hicho  katika mchezo unaofuata wa nusu fainali ya Kombe la mapinduzi dhidi ya Azam FC.




Yanga imetinga hatua hiyo mara baada ya kumaliza vinara wa Kundi B kwa kukusanya pointi nne na kesho Jumatatu itacheza dhidi ya Azam FC.


Kiungo Said Ntibazonkiza tayari amewasili Zanzibar kwa ajili ya kuongeza nguvu na Yanick Bangala, Djuma Shabani na Mukoko Tonombe tayari wameshamaliza mechi yao ya timu ya taifa Januari 6, hivyo wapo tayari hivyo huenda wakawa sehemu ya kikosi kitachocheza mchezo huo.