Staa wa Ufaransa na PSG Kylian Mbappé amefikia makubaliano na Real Madrid ya kusaini mkataba kama mchezaji huru ifikapo majira ya kiangazi, kwa mujibu ripoti kutoka Ujerumani

 




Hii ni habari mbaya kwa PSG ambao walikataa ofa ya Paundi 154 mil, kutoka kwa Real Madrid kwenye majira ya kiangza mwaka jana

 

Mabingwa hao wa Ligue 1 walikataa ofa hiyo wakiwa na matumaini ya kumshawishi mshindi huyo wa kombe la Dunia, kusalia Paris lakini inaonekana dili hilo kukwama baada ya Mbappe kugoma kuongeza mkataba mpya.