Beki wa kulia wa Paris Saint-Germain, Achraf Hakim jana usiku, ameipeleka Morocco hatua ya robo fainali ya Afcon baada ya kufunga goli la ushindi dhidi ya Malawi akifunga kwa faulo matata.

 


Free kick hiyo imemfanya staa mwenzake wa PSG Kylian Mbappé  kuandika kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa Hakim ndiye beki bora wa kulia duniani.

 

Kwenye mchezo huo Malawi walikuwa wa kwanza kufunga kupitia Gabadinho Mhango dakika ya 7’ na goli la kusawazisha kwa Morocco likiwekwa wavuni na Youssef En- Nesyri dakika ya 45.

 

Morroco imetinga hatua kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Malawi ambao wameingia hatua  ya 16 bora kama (best loser).