Timu ya taifa ya Misri imetinga hatua ya Nusu fainali ya michano ya  Afcon baada ya kufanya ‘come back’ ya kibabe dhidi ya mahasimu wao wakubwa Morocco jana Januari 30, na kuibuka na ushindi wa magoli 2-1.

 

Mohamed Salah akishangilia pamoaja na wachezaji wenzake baada ya Misri kutinga hatua ya nusu fainali ya Afcon.

Morocco walikuwa wa kwanza kutisa nyavu za Misri kupitia kwa Sofiane Boufal kwa mkwaju wa penati dakika ya sita vao ambalo lilidumu mpaka mwisho dakika 5 zinamalizika.

 

Misri walianza kulisakama lango la Morocco na kufanikiwa kusawazisha  nahodha wao Mohamed Salah dakika 53.

Mohamed Trezeguet akishangilia baada ya kufunga holi la ushindi dhidi ya Misri.
Mahamoud Trezeguet akishangilia baada ya kufunga goli la ushindi dhidi ya Morocco

 

Baada ya dakika 90 za mchezo kuisha mechi ikiwa sare, zikaongezwa dakika 30 ambapo Mahmoud 'Trezeguet' alifunga bao dakika ya 100 na kuipa uhakika Misri kutinga hatua ya Robo Fainali

 

Misri itacheza na  na wenyeji wa michuani hiyo Cameroon Jumatano Februari 3, kwenye hatua nusu fainali ya kwanza, wakati nusu fainali nyingine itakuwa kati ya Senegal dhidi ya Burkina Faso Jumanne Februari 2.