Klabu ya Yanga leo Januari 19, imecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mbuni Fc na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 mechi iliyochezwa  kwenye uwaznja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha

 


Mabao ya Wananchi yamefungwa na Mukoko Tomombe 'Teacher'  kwa njia ya mikwaju ya  penati katika ya 56’ na 82

 

Yanga imetumia wachezaji wake wengi ambao hawapati  nafasi ya kucheza na pia  mashabiki wa Yanga walifanikiwa kumuona nyota mpya Chiko Ushindi kwa mara ya kwanza akicheza ndani ya uzi wa Yanga.

 


Wananchi wapo Arusha wakijiandaa na mchezo wa ligi kuu ya NBC dhidi ya Polisi Tanzania