Kinda wa Yanga, Denis Nkane alisajiliwa hivi karibuni akitokea Biashara United atakuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja kutokana na kusumbuliwa na Kinena.

 




Nkane alisajiliwa na Yanga kwenye dirisha dogo la usajili akitokea Biashara United, huku kwa sasa akiwa
amecheza mechi mbili za michuano ya Mapinduzi.

 

 

Kiungo huyo aliumia kwenye mchezo wa hatua ya makundi dhidi ya KMKM kwenye Kombe la Mapinduzi.

 


Kwa mijinu wa Gazeti la Championi , Daktari waYanga, Youssef Mohammed, alisema kuwa: “Kwa sasa kuna jumla ya wachezaji wanne ambao ni majeruhi kwenye kikosi.

 

 
“Denis alipata majeraha kwenye mchezo wa mwisho wa makundi ambapo kwa sasa anasumbuliwa na Kinena, tatizo ambalo litamuweka nje kwa muda wa mwezi mmoja.”