Kocha wa
Simba, Pablo Franco, ametetea uamuzi wake wa kucheza bila straika halisi katika
mchezo wao wa Jumatano iliyopita dhidi ya Kagera Sugar, mfumo ambao umekuwa
ukitumiwa sana na kocha wa Man City ya England, Pep Guardiola.
Akizungumza na gazeti la Championi , kocha
Pablo alisema: “Kama kocha, wajibu wangu mkubwa ni kutafuta suluhisho
inapotokea tunapitia changamoto fulani. Kabla ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar
hatukuweza kufunga bao lolote kwa dakika 180 za michezo miwili mfululizo
iliyopita na niliamini tulipaswa kufanya maamuzi ya utofauti.
“Hapo ndipo tulikuja na wazo la
kutumia namba tisa kivuli kwa kujaza viungo wengi na kumtumia Morrison kama
straika wetu, kila mmoja ni shuhuda kuwa kwa kiasi fulani tulifanikiwa
kutengeneza nafasi lakini kwa bahati mbaya hatukufanikiwa kupata mabao.
Katika mchezo huo wa Jumatano iliyopita, Simba
hawakuanza na straika yeyote wa asili huku wakianza na viungo sita ambao ni
Sadio Kanoute, Rally Bwalya, Clatous Chama, Pape Sakho, Mzamiru Yassin na
Bernard Morrison ambaye alicheza kama mshambuliaji.
Chanzo: Championi
0 Maoni