Real Madrid imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya mahasimu wao wakubwa Barcelona kwenye mchezo wa nusu fainali ya Spanish Super Cup uliochezwa huko Saudi Arabia.

 


Madrid walikuwa wa kwanza kutisa nayvu za Barca kupitia Vinicius Jr dakika ya 25, Luuk de Jong alisawazishia Barca dakika ya 41 na kwenda mapumziko wakiwa  sare ya bao 1-1.

 

Kipindi cha pili Mfaransa Karim Benzema alikwamisha mpira ndani ya kimia na kuipa Los Blancos uongozi dakika 72.


Vijana wa Xavi walirejea na kusawazisha kupiti kwa Ansu Fati dakika ya 83' aliyesababisha mchezo  kuongezwa dakika 30 (Extra Time) ili kumpata mshindi.

 

Aliyepeleka kilio kwa Barca alikuwa Federico Valverde ambaye alifunga dakika ya 98' na kuipeleka Reala Madrid Fainali ya Spanish Super Cup

 

Ikiwa ni El Classico yake ya Kwanza kama kocha wa Barcelona Xavi Hernandez amekiri kuwa kwa sasa wapinzani wao wamewacha mbali inabidi wafanye kazi ya ziada kuwafikia Madrid walipo.