Staa wa Manchester United, Cristiano Ronaldo hakufurahishwa na uamuzi  Kocha Ralf Rangnick baada ya kumpumzisha dakika ya 70  nafai yake kuchukuliwa na Harry Maguire kwenye ushindi wa mabao 3-1  mchezo wa ligi kuu  dhidi ya Brentford.

 


Ronaldo alimuuliza Rangnick kwa nini aliamua kumtoa yeye na sio mtu mwingine, akijibu swali la mwandishi baada ya mechi kuisha kocha huyo wa muda wa United amesema alimwambia Ronaldo kuwa amefanya maamuzi hayo kwa maslahi ya timu maana yeye ni meneja

 

"Wiki iliyopita mpaka dakika ya 70 tulikuwa mbele kwa magoli mawili lakini baada ya filimbi ya mwisho matokeo yalikuwa 2-2 sikutaka hali ijirudie tena" alisema Rangnick