Waziri wa mambo ya Ndani wa Australia Karen Andrews amesema mcheza Tenisi namba moja Novack Djokovic  anaruhusiwa kuondoka nchini humo muda wowote na hajashikiliwa kama ambavyo inaripotiwa vyombo vya habari.


 


Djokovic 34 yupo karantini akisubiri rufaa aliyoikata kupinga kufutiwa visa yake kwa, rufani hiyo itasikilizwa jumatatu.


Nchini Serbia kumekuwepo na maandamo kutoka kwa mashabiki wakishinikiza kuachiwa huru kwa mshindi mara 20 wa Grand Slam.

 

Michuano ya Australian Open inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 10 mpaka 30 mwaka huu.