Staa wa Liverpool Mohamed Salah, ameweka wazi kuwa suala ya yeye kuondoka au kubaki kwa majogoo hao wa jiji lipo mikononi mwa klabu hiyo kwa sababu wanajua anachotaka ili kuendelea kusalia kukipiga Anfeld.



Mkataba wa Salah 29, unaisha mwakani 2023 huku wamiliki wa Liverpool wakihaha kuhakikisha wanampa mkataba mpya.

 

“ Naijua klabu, nawapenda mashabiki Nataka kubaki lakini hili lipo nje ya mikono yangu lipo chini yao kwa sababu  uongozi wanajua ninachotaka” amenukuliwa Salah.

 

Imeripotiwa kuwa Salah anataka kulipwa Paundi 300,000 mpaka 350,000, sawa na Bil 1 na ushee za kitanzania, msimu huu tayari amefunga magoli 23 kwenye michezo 26 aliyocheza.

Kwa sasa Salah yupo nchini Cameroon a timu ya taifa ya Misri inayoshirikia michuano ya Afcon