Simba inajitupa uwanjani kucheza na Mtibwa Sugar  Leo Januari 22 ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Mbeya City kwa bao 1-0.




 

 

Timu hizo zinatarajiwa kuvaana katika mchezo wa Ligi Kuu Bara leo Jumamosi saa kumi kamili kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.

 

Simba itawakosa kiungo Jonas Mkude na mshambuliji Kibu Denis kutokana na majeraha, kwa upande wa Mtibwa Sugar Kocha Salum Mayanga amesema anaamini Simba itakuja kivingine lakini wao wamejiandaa kushinda.