SIMBA Queens imeendeleza rekodi ya ubabe mbele ya Yanga Princess kwa kuendeleza vipigo kwenye msimu wao wa nne mfululizo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 katika mchezo uliopigwa  jana Uwanja wa Mkapa Dar es salaam.

 


Simba Queens imeweka rekodi ya kushinda mechi sita kati ya saba ilizowahi kukutana na Yanga kwenye ligi.

 

Ushindi huo umeifanya Simba kurudi kileleni kwenye msimamo wa ligi na kuishusha Fountain Gate ambayo ilikuwa inaongoza kwa alama tisa wakati Simba baada ya kushinda imekusanya alama 11.

Mabao ya Simba yalifungwa na Oppah Clement aliyefunga mawili pamoja na Asha Djafar ambaye pia alifunga mawili huku bao pekee Yanga likufungwa na Aisha Masaka kwa mkwaju wa penalti.