Timu ya Simba leo Januari 13,  imefanikiwa kutwaa ubingwa w kombe la mapinduzi baada ya kuicha Azam Fc kwa bao 1-0 mchezo uliochezwa uwanja wa Amaan, Zanzibar

 


Goli pekee la Simba limefungwa na mshambuliaji Meddie Kagere dakika ya 56’ kwa mkwaju wa penati baaya mlinda mlango wa Azam Fc KIgonya kumfanyia faulu Pape Osmane Sakho.

 


Kwa ushindi huo mnyama Simba amemaliza uteja mbele ya Azam Fc baada ya kupoteza fainali tatu za kombe la mapinduzi.



Mlinda mlango wa Simba Aishi Manula amechaguliwa kuwa Golikipa bora wa michuano hiyo akiwa hajafungwa bao, Pape Sakho amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano hayo na Fowadi Meddie Kagere akiwa ndiye mfungaji Bora.

 

Mchezaji wa bora fainali amechaguliwa beki mkongomani  Inonga Baka