Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF leo Januari 24, limekanusha kumfungulia kesi Polisi kiongozi yoyote wa mpira wa miguu.

 



Kwa mujibu wa taarifa ilitolewa na TFF kupitia kwa Ofisa Habari  na mawasiliano Cliford Mario Ndimbo, masuala yote yanayohusu viongozi wa mpira  wa miguu yamekuwa  yakipelekwa kwenye vyombo vya vinavyohusika na mpira.


 

 Shirikisho hilo linawataka wanaondesha propaganda hizo kuacha  mara moja, kwani hawatasita kuchukua hatua stahiki kwa wote wanaoendelea kusamabaza.  


Mapema siku ya leo kumeibuka taarifa zilizokuwa zikidai Shirikisho hilo limemfungulia Mashtaka Barbara Gonzalez kwa kitendo cha kutoa lugha Chafu wakati wa mchezo wa Simba na Yanga Disemba 11 mwaka jana, baada ya kuzuiliwa kuingia eneo la VVIP na watoto ambao kiutaratibu hawaruhusiwi.