Mlinzi wa kulia wa Timu ya Taifa ya England Kieran Trippier amejiunga na Newcastle United kwa mkataba wa miaka miwili na nusu.



 

Trippier ambaye alikuwa akikipiga Atletico Madrid ya Hispania amsajiliwa kwa paundi  mil. 12 amekuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na matajiri wa Saudia Arabia ambao ni wamiliki wapya wa klabu hiyo.

 

Mchezaji huyo wa zamani wa Spurs ametumia ukurasa wale kwenye mtandao wa Instagram kuonyesha furaha yake baada ya ukamilisho huo kukamilika.


 

Ninafuraha kujiunga na Newcastle kila mtu anajua mashabiki wake ni wakipeee nasubiri kwa hamu kuanza mazoezi na wachezaji wenzangu, na kuingia kucheza kwenye uwanja wa St. James Park.