Unaweza kuwa mwanzo mbaya kwa kwa vigogo wa soka Afrika Kaskazini kwenye michuano ya Afcon inayoendela nchini Cameroon, baada ya Misri kupoteza dhidi ya Nigeria,  Algeria kulazimishwa Sierra Leone sare, leo Tunisia imeangukia pua baada ya kufungwa na Mali kwa bao 1-0 mchezo wa kundi F 

 


Goli pekee la Mali limekwamishwa wavuni na  Ibrahima Kone  dakikia ya 49 kwa mkwaju wa penati baada ya beki wa Tunisia kuunawa mpira ndani ya 18.

 

Nahodha wa Tunisia Wahbi Khazri alikosa mkwaju wa penati dakika ya 77 baada ya mlinda  mlango wa Mali Mounkoro kupangua mkwaju huo.

 

El Bilal Toure alilimwa kadi nyekundu dakika ya 87, na kuwifanya Mali kucheza Pungufu uwanjani, mwamuzi aliingia kwenye mzozo na benchi la ufundi la Tunisia wakiadai alimaliza mchezo kabla ya muda.