Klabu ya Manchester United Imethibitisha kuwa nyumba ya Beki Victor Lindelof  ilivamiwa wakati United ikicheza ugenini dhidi ya Brentford na kuibuka ushindi wa mabao 3-1.

 




Kupitia ukurasa wa Inastagram wa mke wa Lindeloaf, Maja aliindika "kuwa watu wasiojulkana walivamia nyumba yetu (Manchester) wakati wa mechi ya Jumatano tulifanikiwa kujifungia na hakuna aliyepata madhara"

 

Kufuatia kadhia hiyo meneja wa muda wa United, Ralf Rangnick  amesema Mswidishi huyo hatakuwa sehemu ya mchezo dhidi ya West Ham kesho ili  apate nafasi ya kuwa na familia.

 

“Niliongea kwa dakika 25 akanielezea kwa undani kilichotokea  ameomba apate muda kupumzika na familia mimi kama baba naelewa anachopitia hivyo nimempa ruhusa.alisema Rangnick.


Polisi katiaka jiji la Manchester  bado wanaendelea na msako kuwabaini waliohusika na uhalifu huo.