Kiungo wa Arsenal Granit Xhaka ameomba radhi baada ya jana usiku  kutolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo wa nusu fainali ya Carbao Cup dhidi ya Liverpool ulioisha kwa Suluhu.

 


Xhaka alitolewa dakika ya 25 baada ya kumfanyia faulo Diego Jota  na kuifanya Arsenal kucheza pungufu  kwa dakika 65.

Napenda kuomba radhi wa watu wote nawapongeza wachezaji wenzangu kwa kupambana na kumaliza mchezo bila kuruhu goli aameandika Xhaka kwenye ukurasa wake wa Instagram

 

Timu hizo zitarudiana tena kwenye mechi yam kondo wa pili utakaochezwa Januari 20 katika dimba la Emirates, mshindi atavaana na Chelsea kwenye fainali.