Kombe la
Mapinduzi linazidi kushika kasi visiwani Zanzibar ambapo msimu huu timu za visiwani
zinaonekana kujizatiti na kutoa upinzani mkubwa kwa kwa vigogo kutoka Bara kwa
kutandaza soka safi, la mbunu na la kuvutia.
Vigogo hao wa
soka bara licha ya kuwa
na sehemu kubwa ya vikosi vyao
lakini walishindwa kuzibeba pointi
tatu kwenye mechi za jana zikiwa ni za
mwisho kwenye makundi yao na waliambulia pointi moja tu.
Yanga
ndiyo walikuwa wa
kwanza kucheza ambapo walitoshana
nguvu na KMKM kwa kufungana
mabao 2-2 kisha Simba wao
wakashindwa kuziona nyavu za
Mlandege na kutoka nao suluhu.
Kwa
mujibu wa kanuni za Kombe la Mapinduzi zinamtaja kinara wa kundi B ambalo Yanga wamemaliza wakiwazidi KMKM mabao ya kufunga kukutana na kinara wa Kundi A ambapo hadi sasa Azam wakishika nafasi ya kwanza wakiwa na pointi sita huku wakitarajiwa kumaliza leo Jumamosi dhidi ya Yosso Boys.
0 Maoni