Kuelekea mchezo wa Nusu fainali ya kwanza wa Mapinduzi Cup  inayoendelea visiwani Zanzibar kati ya Bingwa Mtetezi yanga ambao watavaana na Matajiri wa Jiji Azam Fc, Wananchi leo itakosa huduma ya kiungo wake  Abubakary Salumu Sure Boy ambaye anaugua Malaria




Pia Yanga itakosa huduma ya winga wake mpya mwenye kasi ya  Denis Nkane aliyeumia katika Mtanange dhidi ya KMKM pamoja na Beki wa Kushoto Yasini Mustafa nae alipata majeruhi katika mchezo uliopita.


Lakini kurejea kwa Fiston Mayele Shaban Djuma na Yanick Bangala kunaipa ahueni Yanga kwenye mchezo huo wa Nusu Fainali utakaopigwa saa 10:15 jioni.