Mchezo wa ligi kuu ya NBC kati ya Coastal Union dhidi ya Yanga umemalizika kwa wananchi kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika dimba la Mkwakwani  jijini Tanga.


Licha ya sehemu ya kuchezea (pitch)  kutokuwa nzuri timu zote zilijaribu kuweka mpira chini na kujarinbu kutafuta nafasi za kufunga, Fiston Mayele ndiye aliyefungua pazia la magoli kwa upande wa Wananchi akifunga goli safi kwa kichwa baada ya kupokea krosi ya Djuma Shabani.

 

Kipindi cha dakika za lala salama  na Saido Ntibazonkiza alikwamisha mpira wavuni akiunganisha mpira wa faridi Musa na kuachia fataki kali na kufanya ubao kusoma 2-0.


Yanga inaendelea kusalia kileleni mwa msimamo na alama 32 baada ya kucheza mechi 12.