Klabu ya Yanga imetumia Sh Mil 50 kufanikisha
usajili wa
mshambuliaji wa Mbeya
Kwanza, Chrispin Ngushi
aliyekuwa akiwindwa
pia na Simba na
kumpa mkataba wa miaka
mitatu.
Ngushi mwenye mabao matatu akicheza michezo 11 ya Ligi Kuu Bara msimu huu, ni wa nne kwa Yanga kusajiliwa kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
Wachezaji
wengine waliosajiliwa
na Yanga na kutambulishwa
ni Salum Aboubakar
‘Sure Boy’ kutoka
Azam FC, Denis Nkane (Biashara United) na Aboutwalib Mshery (Mtibwa Sugar).
Yanga ipo visiwani Zanzibar ikiwa inashiriki michuano ya kombe la mapinduzi na leo wanashuka dimbani kucheza na KMKM.
0 Maoni