Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ally   amesema kuwa, kikosi cha mnyama kipo vyema na kimejiandaa vizuri na mchezo wa Jumapili ikiwa ni pamoja na baadhi ya majeruhi kurejea kikosini.



Akifanya mahojiano na kitup cha redio cha Efm  leo Februari 11, Ahmed  amesema habari njema kwa wanasimba ni kuwa habari njema ni kurejea kwa kiungo Taddeo Lwanga kikosini na wakati ule kulikua na tetesi kwamba angeachwa lakini sio kama taarifa zilivyosambaa.



"Taddeo Lwanga amerejea kikosini, sasa ni mzima ila suala la yeye kuingia kwenye mchezo huu hilo tunamuachia kocha lakini pia kulikua na tetesi kwamba Simba ilitaka kumtema, naomba niweke sawa hapo kwamba sisi tulipata ushauri wa wataalam na madaktari wa timu kwamba tumuache mpaka atakapopona vizuri, na walitupa makadirio kuwa inaweza kuwa Mwishoni mwa mwezi Januari na sasa amerejea tena"