Arsenal imefanikiwa kuondoka na alama tatu muhimu mbele ya Wolverhampton Wanderers baada ya kushinda kwa bao 1-0 kwenye mchezo wa ligi kuu England, ulichezwa usiku wa jana Alhamisi kwenye uwanja wa Molineux, Wolverhampton.


Bao pekee la Gabriel Martinelli dakika ya 25, kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 39 katika mchezo wa 22 na kupanda nafasi ya tano ikiizidi wastani wa mabao Manchester United, ambayo pia imecheza mechi moja zaidi.


Wolves inabaki na pointi zake 34 baada ya kushuka dimbani mara 22 katika nafasi ya nane.

 

Katika mchezo huo Arsenal ililazimika kucheza pungufu baada ya Gabriel Martinelli kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 69.