Arsenal wamevunja mkataba na mshambuliji wao Pierre-Emerick Aubameyang ili aweze kujiunga na Fc Barcelona kwa uhamisho wa moja kwa moja na sio mkopo kama ambavyo ilikuwa awali.

 


Dili la mkopo limekwama baada ya Arsenal kukataa kulipa sehemu ya mshahara wa mchezaji huyo  wa kimataifa wa Gabon, paundi laki 350,000 ambazo ni zaidi ya Tsh Bil 1.8

 

Kuvunja mkataba kumewarahishia kazi Barca na kukabaliana na Auba ambaye amekuwa mchezaji huru masaa matatu kabla ya dirisha la usajili kufungwa.


Aubameyang amesaaini mkataba wa miezi sita wenye nyengoza ya kuongeza mwaka mmoja.