Staa wa kimataifa wa Gabon Pierre-Emerick
Aubameyang amethibitisha kuwa ameondoka katika klabu ya Arsenal kwa sababu ya kutoelewana na kocha wa timu hiyo
Mikael Arteta.
Nahodha huyo
wa zamani wa Gunners leo akiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari baada ya
kutambulishwa rasmi na Barcelona ameweka
wazi kuwa uhusiano kati yake na Arteta ulianza
kwenda kombo baada ya kumvua unahodha kutokana na makosa ya kinidhamu.
Aubameyang
alitoroka kambini Dubai na kwenda Hispania kukamilisha dili hilo bila idhini ya klabu siku
ya mwisho kabla ya usajili kufungwa.
“Nafikiri
tatizo ilikuwa kwake hakuwa na furaha na mimi akamua kufanya maamuzi, kwa
upande wangu kilikuwa kipindi kigumu
lakini nilitulia, huwa inatokea kiwenye mpira lakini yalishapita”
Akizungumzia
kuhusu klabu yake mpya Auba amesema ni nafasi ambayo alikuwa akisubiria kwa
hamu kubwa na pindi ilipotokea hakusita kuichukua “nilikuwa na ndoto za kucheza
La liga ni nafasi adhimu kwangu kuipata kila mmoja anajua Barcelona ni klabu bora duniani.
0 Maoni