Leo Februari 2, mtanange wa  nusu fainali ya kwanza ya michuano ya soka ya mataifa barani Afrika AFCON inatajiwa kupigwa kati ya Burkina Faso dhidi ya Senegal kuwania nafasi ya kutinga hatua ya fainali ambayo utachezwa jumapili.

 


 

Timu zote mbili hazijawahi kutwaa ubingwa wa Afrika, Senegal wamecheza fainali mbili za michuano hii na zote wamepotea walicheza fainali ya kwanza mwaka 2002 walifungwa kwa mikwaju ya penati 3-2 dhidi ya Cameroon na mwaka 2019 walifungwa bao 1-0 na Algeria.

 

Burkina Faso ambao pia ni washindi wa 3 wa fainali zilizopita  za mwaka 2019 wanaiwinda fainali ya pili baada ya kucheza fainali yao ya kwanza kwenye michuano hii mwaka 2013 fainali ambayo walipoteza kwa kufungwa bao 1- 0 na timu ya taifa ya Nigeria.

 

Je nani ataibuka mbabe kwenye mchezo huu wa kutafuta nafasi ya kuingia Fainali majibu ni saa leo 10:00 usiku.