Wenyeji wa michuano ya Afcon jana usiku kushinda nafasi ya mshindi wa tatu kwa kuibuka
na ushindi kwa penati 5-3 baada ya kutoka sara ya 3-3 dhidi ya Burkina Faso
mchezo uliopigwa uwanja wa Ahmadou-Ahidjo in Yaounde, Cameroon.
Burkina Faso walianza vema kwa mchezo huo kwani mpaka dakika
ya 50’ walikuwa mbele kwa mabao 3-0 mabao
yakifungwa na Steeve Yago dakika ya 24, bao la kujifunga la kipa wa Cameroom André
Onana dakika ya 43, na Djibril Outtara
dakika ya 49.
Cameroon waligeuza kibao na kuanza kusawazisha kuptia kwa
Bahokem na magoli mawili ya haraka haraja ya kinara wa mabao kwenye michuano ya
mwaka huu nahodha wa Vincent Aboubakar na kulazimisha mchezo kuongezea dakika
30 ili kumpata mshindi.
Dakika hizo zilimalizika hakuna mbabe ndipo mikwaju ya penati ikaamua mchezo huo na Cameroon kuibuka kidedea kwa kushinda penati 5-3 kutwaa nafasi ya mshindi wa tatu.
Mchezo wa Fainali ya michuano hiyo unachezwa leo kati ya miamba ya Afrika Magharibi Senegal ambao wataongozwa na mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane dhidi ya Misri ambayo itaingozwa na mchezaji wa Liverpool Mohamed Salah.
0 Maoni