Staa  wa tennis Mserbia Novak Djokovic amesema yupo tayari kukosa michuano mikubwa ijayo ya tennis (French open na Wimbledon open) kama itakuwa lazima kuchanja kama ilivyokuwa kwenye michuano ya wazi ya Australian 2022 yaliyomalizika mjini Melbourne mwezi Januari 31.

 


"sijawahi kupinga chanjo hata siku moja kwa sababu nilipokuwa mdogo nilipata chanjo kadhaa, lakini kila siku naunga mkono uhuru wa mtu kujiamulia kitu gani kiingine kwenye mwili wake na nipo tayari kulipa gharama ya kutoshiriki kwenye mashindano yajayo kisa kubaki na msimamo wangu wa kutochanjwa "amesema Djokovic

 

Djokovic mwenye umri wa miaka 34, anayeshuka nafasi ya kwanza kwa ubora wa viwango wa tenisi duniani kwa upande wa wanaume akiwa mataji makubwa 20 ya tennis (Grand Slams) alizuiliwa kushiriki kwenye michuano ya wazi ya Australian mwaka 2022 baada ya kuzuiliwa kutokana na kutochanjwa chanjo ya Uviko 19 na kunyang'anywa pasi yake ya kusafiria ya kuingia nchini humo.