Klabu ya Everton ya England imekamilisha usajili wa Dele Alli, kutoka Tottenham Hotspurs dakika chache kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo la usajili jana saa sita usiku, kwa dau la paundi mil.40 kwa mkataba wa miaka miwli na nusu.

 




Delle ambaye ameichezea Spurs mechi 269 na kufunga magoli 67 tangu alipojiunga na timu 2015, anaungana na kocha mpya Frank Lampard pamoja na Donny van de Beek alijiunga kwa mkopo hadi mwisho wa msimu akitokea Mancheter United.


 Nina shauku kubwa ya kucheza mechi ya kwanza nikiwa na jezi ya Everton kuisadia klabu hii kufika malengo na  chini ya kocha mpya Frank Lampard asema Dele.

Huenda mchezaji huyo wa kimataifa wa England akawa sehemu ya mchezo wa ligi kuu England dhidi ya Newcastle United Jumanne ijayo.